sw.news
444

Ukinzani Zaidi Kutoka Kwa Kasper: Waprotestanti Na Wakatoliki Ni "Kanisa Moja"

Akizungumza kwa ukinzani, Mprotestanti halisi Kadinali Walter Kasper amedai kwamba Wakatoliki na Waprotestanti ni wanachama wa "Kanisa moja Takatifu la Kristo" lakini wakati uo huo "sio katika ushirika kamili.

Akiandika kwenye mtandao wa katholisch.de (Aprili 23), Kasper aliliwacha wazi jinsi ambavyo mtu anaweza kuwa mwanachama wa mwili wa Kristo huku asipokuwa mwanachama kamili wa mwili huo.

Kaw msingi huu anaomba kuwe na Ekaristi kwa Waprotestanti, haswa kwa ndoa kati ya watu wa dini tofauti kwani husemekana kwamba wao huunda "kanisa la kinyumbani".

Lakini Kasper hajibu swali ni kwa nini Waprotestanti halisi wangetaka kupokea Ekaristi Takatifu. Au: Iwapo mtu asiye Mkatoliki ana mvuto wa kweli kwa Ekaristi ya Kikatoliki, ana wajibu wa kidini na kimaadili kujiunga na ushirika huu.

Kupokea Ekaristi huku akiukataa Ushirika kunakinzanam, hakumfai Mkristo ambaye ameitwa kuishi katika ukweli wa Kristo ambako hakuna ukinzani.

Picha: Walter Kasper, © Mazur, catholicchurch.org.uk, CC BY-NC-SA, #newsLpfantvvos