sw.news
455

Kadinali Wa Francis Amlinda Askofu Msaidizi Anayekumbwa Na Utata

Askofu msaidizi Juan Pineda wa Tegucigalpa, Honduras, juishi maisha ya kifahari ambayo huhusisha umiliki wa magari kadhaa ya kifahari na safari za mara kwa mara za ndege za kifahari, Edward Pentin …Zaidi
Askofu msaidizi Juan Pineda wa Tegucigalpa, Honduras, juishi maisha ya kifahari ambayo huhusisha umiliki wa magari kadhaa ya kifahari na safari za mara kwa mara za ndege za kifahari, Edward Pentin aliripoti (Aprili 27).
Hata hivyo, Pineda hubaki katika wadhfa wake kwa ulinzi wake Kadinali wa Tegucigalpa Oscar Rodríguez Maradiaga, rafiki wa karibu wa Pineda ambaye pia ni mratibu wa Baraza la Makadinali na mwanapropaganda wa itikadi za "ufukara" za Francis.
Kulingana na Pentin, Pineda alihusika katika kutoweka kwa Dola milioni 1.3 ambazo zilitolewa na serikali ya Hondura kwa miradi ya msaada ya Kanisa. Fedha hizo ziliwekwa ila hazikupitia utaratibu wa kawaida wa kifedha wa dayosisi hiyo na hatimaye "zikatoweka".
Pineda alijaribu kueleza zilivotumika pesa hizo, lakini ripoti yake haikutoa hati za invoisi, vocha wala hati zozote.
Mwezi uliopita, Pentin alifichua kwamba Pineda amekashifiwa na wanaseminari wa zamani kwa shutma za dhulma za kishoga.
Picha: Juan Pineda, © House Committee on …Zaidi